Thursday, August 18, 2016
VIJANA ELFU 18 KUSOMA UFUNDI STADI KWA SIMU KUPITIA AIRTEL FURSA VSOMO

VIJANA ELFU 18 KUSOMA UFUNDI STADI KWA SIMU KUPITIA AIRTEL FURSA VSOMO


Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel na VETA imeingia mkoani Arusha kuendelea kutoa uelewa kwa vijana kukamata FURSA na kusomo kozi mbalimbali toka VETA kupitia mfumo wao wa simu ujulikanao kama VSOMO. hadi sasa zaidi ya vijana elfu kumi na nane nchini wamejisajili kusoma kwa mfumo huo wa simu za mkononi huku mikakati yao ikiwa ni kuongeza kozi 10 zaidi ili wanafunzi kuendelea kujisomea.

Hayo yamebainishwa na  Mkuu wa mauzo kanda ya kaskazini  Bw, Brighton Majwala wakati alipoongea na wajasiliamali na madereva bodaboda  waliokusanyika stand kuu  Arusha jana,   
“Airtel na Mamlaka ya ufundi stadi VETA lengo letu ni kuwafikishia elimu ya ufundi vijana wengi nchini, upande wetu Airtel tunahakiksha mtandao upo vyema ili vijana waweze kusoma bila kukwama, hadi leo hii tayari vijana zaidi ya milioni 18 wameshakamata FURSA hii kwa kupakua aplikesheni au mfumo huu wa VSOMO katika simu zao” alieleza Bw Majwala

Majwala aliendelea kusema kuwa “mpango wetu Airtel na VETA ni  kuongeza uelewa kwa  vijana ili wasome kozi zilizopo sasa ikiwemo ya  ufundi piki piki, umeme wa nyumbani, ufundu simu, ufundi wa aluminium, utaalam wa masuala ya urembo, pamoja na ufundi wa kuchomea vyuma”.

Kwa upande wake Meneja  Uhusiano wa Airtel alisema “kutokana na VSOMO kuwa na idadi kubwa ya vijana waliojisajili  tayari Airtel kwa kushirikiana na wadau wetu VETA tuko katika utekelezaji wa kuongeza kozi zingine zaidi ya kumi ili kuongeza wigo wa kuchagua pamoja na kuongeza  idadi ya wanaosoma na kuhitimu”. alieleza mmbando

“tunampango wa kuongeza kozi zingine 10 kabla ya mwezi wa 12 ambapo sasa hivi tayari VETA wako katika utaratibu wa kuzifanyia kazi kozi hizo ili ziweze kuingia katika mtandao” alisema Mmbando

 “Mradi wa VSOMO ni sehemu ya mpango wa Airtel FURSA wenye lengo la kuwawezesha vijana pamoja na kutimiza kauli mbiu ya  “Airtel the smartphone network” kwa kujipatia elimu ya ufundi stadi toka VETA kwa smartphone zao” alisisitiza Mmbando

Airtel kwa kushirikiana na  VETA nchini ilizindua mfumo wa masomo ya ufundi stadi kwa njia ya mtandao VSOMO mwezi Julai 2016 ambapo mpaka sasa  tayari mfumo huu umetambulishwa  katika mikoa ya Dar es salaam, Mbeya, Arusha, Morogoro na Mwanza lakini kutokana na uhitaji mkubwa kwa  vijana tayari mfumo huo umepokea maombi ya vijana toka mikoa 25  kwa kupakua mfumo/aplikesheni hiyo hiyo na kuomba kusoma kwa njia ya simu za Airtel.

Chanzo: Michuzi Blog

Saturday, August 6, 2016
Dhana ya Mikopo na Madeni

Dhana ya Mikopo na Madeni

Na: Albert Sanga, Iringa.
Kumekuwa na changamoto kubwa kwa waliojiajiri na walioajiriwa kuhusu dhana ya mikopo na madeni. Licha ya kwamba wakati mmoja hadi mwingine, wengi wetu tumepata kuwa na mikopo au madeni; ni wachache wanaotambua maana halisi ya mikopo na madeni na namna mambo haya mawili yanavyotakiwa kwenda nayo katika maisha ya kiuchumi.
Tuchukulie mfano wa wafanyakazi. Wafanyakazi wengi huwa wanajikuta wakiishiwa mishahara yao kabla hata ya tarehe ya kupokea mshahara mwingine. Wakishamaliza mishahara yao huwa wanajikuta hawana namna ya kumudu bejeti zao, ikiwemo chakula na usafiri; hivyo wanapata mbinyo wa kuazima fedha, huduma au bidhaa kutoka kwa wenzao, katika maduka na kutoka kwa watu binafsi.
Wakishaazima hizo fedha, huduma au bidhaa; mioyo yao inasuuzika, wanamalizia siku zilizobaki kabla ya mshahara. Mshahara unapotoka wanajikuta wanatakiwa kulipa madeni yao, hivyo wengi wao huwa wanaanza kulipa yale madeni kisha inayobaki ndio wanaanza kutumia matumizi mengine. Mtindo unakuwa ni ule ule wa kuishiwa kabla ya mwisho wa mwezi. Kwa kadri mfanyakazi huyu anavyoendelea kukopa madeni kwa mtindo wa namna hii; anaendelea kuzalisha mfumo wa utegemezi unaokua. Ukifuatilia utabaini kuwa kama mwezi huu mshahara ulikuwa unaisha tarehe 20, basi mwezi ujao utaisha tarehe 15, na unaofuata utakuwa unaisha tarehe 10!Mwisho wa siku mshahara wa mfanyakazi huyu usishangae kuona unaisha tarehe 2 ya mwezi! Kwa nini wafanyakazi na watu wengine waendelee kuishi maisha ya aina hii wakati fedha inapita mikononi mwao? Natambua wengi watasema tatizo ni kuwa mishahara wanayolipwa haitoshi, lakini ukweli ni kwamba tatizo kubwa ni kwamba, wengi hawaelewi namna ya kutumia fedha na jinsi ya kumudu madeni na mikopo.
Kanuni inasema kwamba kila fedha inayopita mkononi mwako unatakiwa kuichukulia kama mbegu. Ikipita shilingi kumi ni lazima itoke mikononi mwako ikiwa zaidi ya shilingi kumi. Hapo ndipo ilipo akili ya matumizi ya fedha. Kwa namna maisha yalivyo na halihalisi ya mishahara mingi ilivyo ni vigumu kukwepa suala la kukopa (na hata madeni).
Kwa ujumla hakuna ubaya wa kukopa, lakini kuna tofauti kati ya mkopo na deni. Mkopo ni fedha ama mali inayoazimwa kutoka kwa mtu ama kutoka kwa taasisi; kwa makubaliano ya kurejeshwa katika kipindi fulani; kwa madhumuni ya matumizi ya kuzalisha fedha zaidi ama mali zaidi. Wakati deni ni a) Fedha ama mali iliyoazimwa kwa ajili ya matumizi yasiyozalisha fedha ama mali zaidi b) deni ni mkopo uliopita muda wa makubaliano ya kulipwa.
Ndio maana mtu akienda kukopa fedha benki (kwa madhumuni ya kufanyia biashara) utasikia yule bwana ana mkopo, lakini akishindwa kurejesha mkopo ule kwa wakati uliopo kwenye makubaliano; utasikia yule bwana ana deni! Bahati mbaya ni kwamba kuna watu wengi sana ambao huwa wanachanganya kati ya deni na mkopo.
Wengi wana madeni lakini utasikia wanasema wana mikopo. Mtu anachukua fedha benki kwa dhamana ya mshahara wake kisha fedha hiyo anakwenda kununulia seti ya runinga, sofa na kununulia viwalo, halafu anajifariji kuwa ana mkopo, la hasha! Hilo ni deni. Wengine huchukua fedha benki na kununulia magari ya kutembelea nao hujifariji kwamba wana mikopo; sio kweli hawa ni kwamba wana madeni. Tena hawa wenye kuchukua fedha na kununulia magari ya kutembelea ambayo hayawaingizii chochote zaidi ya kuwalamba fedha zao; wanatakiwa kuyaita “madeni ya kutembelea” na sio magari ya kutembelea.
Katika nukta hii, namna nzuri ya kutumia fedha ni pamoja na kutambua vema nafasi ya mkopo na deni kwako. Unaamini nini kuhusu mikopo na madeni? Una uthubutu na tabia gani linapokuja suala la kudaiwa? Unahimili vipi madeni yako? Haya ni mambo ya kuyajua na kuyarekebisha yakae katika uelekeo sahihi kwa sababu yanaamua sana namna unavyoweza kutumia fedha zako.
Kukopa ni suala zuri sana. Biashara zote duniani zilianzishwa, haunzishwa na zitaendelea kuanzishwa kwa kutumia mikopo. Iwe umechukua hela mfukoni mwako na kuanzisha biashara huo ni mkopo, iwe umepewa fedha, huo ni mkopo kwa biashara yako.
Hata kama mkopo huo hauna riba wala hauhitaji kurudishwa hilo haliondoi uhalisia wa kwamba ni mkopo na katika mizania ya kihasibu mtaji wa kila biashara unatakiwa kuonesha kuwa mtaji wa mwanzo ni mkopo. Hata watu binafsi, iwe ni walioajiriwa ama laa, wenye cha kufanya ama wasio na cha kufanya; ukweli ni kwamba kuna wakati kwenye maisha utapungukiwa na utahitaji kukopa.
Unaweza kukopa benki, kwenye taasisi nyingine ama kwa mtu binafsi, kote huko ni kukopa. Imani yako kuhusu mikopo itaamua sana namna unavyotumia fedha zako katika kulipa ama kutokulipa. Bahati mbaya ni kwamba tunao watanzania wengi ambao hawataki hata kidogo kusikia habari za mikopo.
Hawa utawasikia wakisema, “Mikopo haina maana”, “Kukopa ni umasikini”, “Ukitaka kufilisika jaribu kukopa”. Kama muhusika anaamini hivi uwe na uhakika kwamba ufahamu wake utapeleka taarifa katika ubongo inayoonesha kwamba mkopo ni utumwa!
Sheria ya uvutano wa kimaumbile (Law of attraction) inasema kwamba chochote anachokiogopa mtu hutokea na chochote anachokiogopa mtu hukiabudu na chochote mtu anachokiabudu hudhihirika. Mtu anaeamini kuwa mikopo haifai ikitokea amekopa atakachojitahidi ni kuhakikisha kuwa anahangaika kuulipa mkopo huo ama deni hilo haraka haraka.
Ikiwa mtu huyu ni mfanyakazi ndio atarudi kule mwanzo ambapo kila akipata mshahara atakuwa anakimbilia kurejesha deni analodaiwa. Kinachotokea? Ni kwamba ataendelea kukopa tena na tena na kuendelea kuwa katika utumwa wa madeni na mwisho wa siku akishalemewa atajidhihirishia yeye mwenyewe imani yake ya kwamba kukopa ni utuwa na mateso.
Bahati mbaya wapo wazazi ambao huwaaminisha watoto wao tangu wakingali wadogo ama wakiwa makazini ya kwamba mikopo ni mibaya. Hata wale wanaokopa kupitia makato ya mishahara yao hawawi salama ikiwa wana imani mfu kuhusu mikopo na madeni. Kwa sababu aliyechukua mkopo na kwenda kununua gari ama kununua fenicha za ndani, siku mshahara unapoanza kukatwa na kujikuta haumtoshelezi atageuka na kuanza kunung’unikia madeni kwa ukali wa makato anayoyapata.
Nini maana yake mambo hayo ya madeni na mikopo? Kumbuka kwamba tunaangalia namna ya kuwa na matumizi mazuri ya fedha. Na nimesema kwamba matumizi mzuri ya fedha ni kutumia fedha katika mtiririko unaokuimarishia uchumi wako na sio kukudidimza.
Sasa, kuna wakati katika maisha unaweza kupitia katika changamoto ya madeni. Huenda ulichukua fedha eidha kwa mtu ama katika taasisi kwa lengo zuri la kuzalisha, lakini mambo yakaenda mrama na ukajikuta mkopo umegeuka kuwa deni na huna namna ya kulipa kwa wakati husika. Lakini pia huenda ulichukua fedha na kuielekeza katika matumizi ya ‘kimadeni-madeni’ na unatakiwa kulipa. Walisema waswahili ya kwamba dawa ya deni ni kulipa; hilo ni kweli lakini unatakiwa kulipa deni lako na wakati huo huo uchumi wako uimarike.
Kama ulichukua mkopo benki kwa dhamana ya mali zako; hilo nitalileta kwa kina zaidi katika makala yenye kichwa, “Wajasiriamali na jinamizi la mikopo”. Lakini kote kote, iwe ni kutoka benki, iwe umekopa kwa mtu ama iwe umekopa dukani (na ukajikuta una deni) ni lazima sana uhakikishe unalipa kwa akili.
Kuchukua mshahara wote na kulipa madeni hakutakusaidia zaidi ya kukuangamiza. Kuchukua faida yote na kuipeleka kwa wadeni nako kutakuachia umasikini. Ukiwa katika hali hii ni lazima uzikumbuke tabia za kitajiri; kuhakikisha unatenga kwanza akiba kisha mengine yanafuatia.
Hata kama kuna mbinyo mkali kiasi gani ili ujikwamue na madeni ni lazima uhakikishe unatenga sehemu ya mshahara ama faida yako kwa ajili ya akiba (nap engine uwekezaji) na inayobaki ndipo iende kwa kulipa madeni na matumizi ya kawaida (yale matumizi yasiyozalisha). Kujua namna nzuri ya kutumia fedha ni pamoja na kuwa imara na mwenye msimamo dhidi ya wanaokudai.
Wanaokudai wanaweza kuwa na vishondo vikubwa kweli kweli, wanaweza kuwa na matisho makali kweli kweli, lakini muda wote jitahidi kuvumilia vishondo na matisho yao na kamwe matisho na vishindo vyao visikutoe kwenye kanuni hii, “Madeni yote yalipwe baada ya kutenga akiba”.
Kwa wale waamini wanaozingatia masuala ya sadaka, kanuni hii inanyumbuka na kuwa “Madeni yote yalipwe baada ya kutenga sadaka na akiba”. Madeni ni changamoto na ni kitu ambacho kinatakiwa kuchukuliwa kama kipindi cha mpito kwa mtu yeyote anaepambana kuimarisha uchumi wake.
Kwenye kitabu cha The Richest Man In Babylon; tunapewa maarifa kwamba haijalishi upo kwenye madeni makubwa na magumu kiasi gani, njia rahisi ya kujikomboa kiuchumi ni kuhakikisha unatenga si chini ya asilimia kumi ya kila fedha unayoipata; na kisha kuanza kuitumia ile fedha uliyotenga kwa ajili ya kuwekeza na kuzalisha.
Sote tunastahili ushindi wa kifedha na kiuchumi.
‪#‎PoweredBySisiVijanaTanzania‬

Friday, August 5, 2016
Sisi Vijana Tanzania

Sisi Vijana Tanzania

We have the pleasure to introduce ourselves as one of the becoming leading pioneer organization dedicated and engage in providing diversified opportunities for the youth within the scope of Talent Promotion and Development represented by energetic, dynamic and young team.

Our Mission is to improve the youth's quality of life by bringing upwards opportunities. We are determined to provide range of quality and standardized programs that will enable the youth to develop their individual and social identity in a beneficial way towards the society.

Thursday, August 4, 2016
Bunge la Awamu ya tano Lapitisha Sheria ya Kuanzishwa Baraza La Vijana

Bunge la Awamu ya tano Lapitisha Sheria ya Kuanzishwa Baraza La Vijana

Je, Serikali ya awamu ya Tano italiona hili....?
Serikali tangu awamu zilizopita ilitarajia kuanzisha Baraza la Vijana litakalo kuwa chombo cha vijana kitakacho waunganisha Kitaifa bila kujali itikadi zao za Kisiasa,Imani zao za Kidini wala tofauti zao za Rangi,hayo yaliwahi kusema pia Na Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo aliyekuwepo awamu ya nne Mhe.Fenella Mukangara alipokuwa akisoma Muswada wa Sheria ya Baraza la Vijana Tanzania Bungeni Mjini Dodoma.
Mheshimiwa Mukangara alisema Baraza hilo litaisaidia Serikali kuweza kuwafikia vijana kwa urahisi na kusikiliza shida zao pamoja na kutoa ufumbuzi wa hoja mbalimbali za vijana.Hata hivyo chimbuko la Muswada huo ni katika kutekeleza Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya 2007,Ibara ya 3 Sehemu ndogo ya 11 inayosema kwa uwazi Serikali itawezesha kuundwa kwa Baraza Baraza la Vijana na kuanzisha mfumo wa kisheria ili kuliwezesha kufanya kazi.
“Madhumuni ya Muswada huu ni Kutunga Sheria ya Baraza la Vijana Tanzania(The Youth Council of Tanzania 2015) ili kuwa na chombo cha Kitaifa cha kuwewezesha vijana kujadili masuala yao,kutambua majukumu yao,kukuza maadili mema,kukuza moyo wa umoja ,uzalendo,uwajibikaji na kujitolea kwa malengo chanya miongoni mwao katika nchi yetu,”alisema Mhe.Mukangara.
Mbali na hayo katika sehemu ya pili kifungu cha 4-15 cha Muswada huo unaeleza juu ya masharti mbalimbali kuhusu Uanzishwaji,Uanachama,Muundo na kazi za Baraza.Pia sehemu hii imefafanua Mamlaka ya Baraza na vyombo vya utendaji katika ngazi ya Taifa,Mkoa na Wilaya. ‪#‎BadoNajiulizaJe‬,Mhe.Magufuri ‪#‎Analionahili‬?